Tuesday, March 2, 2010

MWALIMU MZURI ANATAKIWA AWE NA VIGEZO GANI?

1. Kuipenda sanaa au taaluma yako( unayofundisha).

2. Kuelewa kikamilifu manufaa na umuhimu wa taaluma yako kiujumla.

3. Kuwa na tabia ya kujumuika na wataalamu(waalimu) mbalimbali pale upatapo nafasi.

4. Kujua namna ya kukabiliana na vipingamizi vinavyo zuia malengo yako pamoja na yale ya wanafunzi wako.

5. Jaribu kuwafundisha wanafunzi wako ili waje kuwa bora kuliko wewe.

6. Wakati wote endelea kujifunza na kuyaishi yale unayofundisha ili uwe dira kwa wengine.

7. Ni vizuri na muhimu kuwaelewa wanafunzi wako kisaikolojia(tabia zao kwa ujumla).

8. Wapongeze wanafunzi pale wanapostahili pongezi.

9. "Fundisha yale mwanafunzi anayopaswa kujifunza"- Sensei Jean Claude Van Damme

10. "Siku zote kumbuka fikra na makusudio yako wakati ulipokuwa ukianza mafunzo"- Meijin Funakoshi G.

No comments:

Post a Comment