Friday, March 12, 2010

BAADHI YA MITINDO ITUMIKAYO KATIKA KUMITE

1)Kake no sen

Mpinzani wako amekwisha kusudia kuja na shambulizi na
amekwisha ingia kwenye ngome yako, pasipo kukinga
unamuwahi na pigo(haraka sana) kabla hajamaliza shambulizi lake.

2)Tai no sen(Sen no sen)

Wakati mpinzani wako anaanza kuvurumisha pigo lake,
unambabatiza na kinga(kabla hajamaliza shambulizi),
na kumuwahi yeye papo hapo.

3)Go no sen

Mpinzani wako amekwisha shambulia, umekwisha kinga au umemkwepa
na kuanza kurudisha mashambulizi kwenye nafasi zitakazo patikana.
Hapa unamruhusu amalize mashambulizi yake kisha unaanza wewe.


Aina ipi ni nzuri kutumia itategemea na mpiganaji kwani
wapiganaji wengi hutofautiana katika matumizi ya hizi mbinu.

No comments:

Post a Comment