Friday, February 19, 2010

FALSAFA ZA O'SENSEI

MIONGOZO 22 YA MEIJIN GICHIN FUNAKOSHI

1. Karate huanza na kumalizika kwa nidhamu.
2. Daima fikiri kiubunifu.
3. Fikra huja kabla ya mwili.
4. Jiweke tayari kuwa huru kifikra.
5. Jitambue kwanza ndio uwatambue wengine.
6. Karate ni muongozo wa haki na inapaswa kutumika hivyo tu.
7. Sogea kufuatana na mpinzani wako.
8. Kamae ni kwa wanafunzi wapya na shizentai ni kwa wazoefu.
9. Usifikirie kwamba inabidi ushinde ila fikiri kwamba hupaswi kushindwa.
10. Karate si katika Dojo peke yake.
11. Husisha karate katika kila jambo ulifanyalo, wakati wote fikiri kuitumia miongozo hii kila siku.
12. Mafunzo ya karate ni ya wakati wote wa maisha yako.
13. Karate ni kama maji ya moto, yasipoendelea kupashwa moto au kuhifadhiwa na joto lake, hupoa.
14. Mara tu utokapo nyumbani, una wapinzani zaidi ya elfu moja.
15. Hakuna shambulio la kwanza kwenye karate.
16. Elewa tofauti ya sehemu zenye madhara na zisizo na madhara.
17. Uzembe huja kabla ya ajali.
18. Fikiri mikono na miguu yako kuwa kama sime.
19. Kumbuka vipengele vigumu na vyepesi kwenye kata.
20. Karate ikifanyika vyema ni tofauti na kombati(struggle fighting).
21. Jihadhari na matendo yako, usije ingia matatani.
22. Mafunzo ya kata si uhalisi wa jambo lenyewe.

No comments:

Post a Comment