Friday, February 19, 2010

FALSAFA ZA O'SENSEI

MIONGOZO 22 YA MEIJIN GICHIN FUNAKOSHI

1. Karate huanza na kumalizika kwa nidhamu.
2. Daima fikiri kiubunifu.
3. Fikra huja kabla ya mwili.
4. Jiweke tayari kuwa huru kifikra.
5. Jitambue kwanza ndio uwatambue wengine.
6. Karate ni muongozo wa haki na inapaswa kutumika hivyo tu.
7. Sogea kufuatana na mpinzani wako.
8. Kamae ni kwa wanafunzi wapya na shizentai ni kwa wazoefu.
9. Usifikirie kwamba inabidi ushinde ila fikiri kwamba hupaswi kushindwa.
10. Karate si katika Dojo peke yake.
11. Husisha karate katika kila jambo ulifanyalo, wakati wote fikiri kuitumia miongozo hii kila siku.
12. Mafunzo ya karate ni ya wakati wote wa maisha yako.
13. Karate ni kama maji ya moto, yasipoendelea kupashwa moto au kuhifadhiwa na joto lake, hupoa.
14. Mara tu utokapo nyumbani, una wapinzani zaidi ya elfu moja.
15. Hakuna shambulio la kwanza kwenye karate.
16. Elewa tofauti ya sehemu zenye madhara na zisizo na madhara.
17. Uzembe huja kabla ya ajali.
18. Fikiri mikono na miguu yako kuwa kama sime.
19. Kumbuka vipengele vigumu na vyepesi kwenye kata.
20. Karate ikifanyika vyema ni tofauti na kombati(struggle fighting).
21. Jihadhari na matendo yako, usije ingia matatani.
22. Mafunzo ya kata si uhalisi wa jambo lenyewe.

Friday, February 5, 2010

THE ' BLACK PEARL '

NINI MAANA YA KUMITE ?

Sehemu nyingine ya mafunzo ya karate hujumuisha makabiliano baina ya wanafunzi, hii kwa neno
la kijapani huitwa kumite. Kumite hufundishwa kwa hatua mbalimbali kutegemea na staili ya karate.

Kimsingi wanafunzi hujifunza ustadi sahihi wa kushambulia na kuyakabili mashambulizi katika mikanda
ya awali kabla ya kuruhusiwa kukabiliana wakiwa huru kushambulia na kujikinga na mashambulizi.

Lakini watu wengi hapa nchini hufundisha kinyume na taratibu hizi za kitaalam.
Mbaya zaidi wanafunzi hufundishwa kushambulia pasipo na tahadhari.
Mashambulizi ya karate ni lazima yadhibitiwe na yule anayeshambulia
ili kuondoa hatari kama kifo, kuvunjika n.k. Kuna baadhi ya wakufunzi wa karate ambao wana uwezo
mkubwa wa kutoa uhai wa mtu kwa pigo moja tu. Watu wa namna hii wanaelewa hatari iliyopo katika
kumite na siku zote hudhibiti mashambulizi yao kuepusha hizo hatari ikiwa ni pamoja na kuifanya
karate kama sanaa ambayo mtu yeyote ataweza kujifunza pasipo kujali jinsia, umri, umbo au nguvu
aliyonayo.

Tukirudi kwenye falsafa ya karate kumite niliyo izungumzia hapo juu ni 20% ya kumite halisi
katika karate. Asilimia themanini iliyobaki ni mapigano baina na wewe na madhaifu yako . Hii ndiyo
kumite ya kweli inayo kamilisha maana ya karate-do. Kila mtu ni mdhaifu wa jambo fulani, laweza
kuwa moja au zaidi. Hivyo basi ni vema tukaishi tukiyapunguza madhaifu yetu katika safari ya maisha
yetu.



MSIBA WA KARATEKA SAMSON MWAMANDA

Tunasikitika kutangaza kifo cha karateka mwenzetu, Samson Mwamanda (green belt) aliyefariki
dunia ghafla usiku wa kuamkia tarehe 27/01/2010 baada ya kuugua kwa muda mfupi.
Ijapokuwa sisi tulimpenda sana lakini Mungu alimpenda zaidi.
Tunatoa pole kwa familia, ndugu jamaa na marafiki wa marehemu.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi.
Amina



Pichani mdogo wetu Samson Mwamanda wa kwanza kutoka kulia(walio kaa)