Friday, February 5, 2010

NINI MAANA YA KUMITE ?

Sehemu nyingine ya mafunzo ya karate hujumuisha makabiliano baina ya wanafunzi, hii kwa neno
la kijapani huitwa kumite. Kumite hufundishwa kwa hatua mbalimbali kutegemea na staili ya karate.

Kimsingi wanafunzi hujifunza ustadi sahihi wa kushambulia na kuyakabili mashambulizi katika mikanda
ya awali kabla ya kuruhusiwa kukabiliana wakiwa huru kushambulia na kujikinga na mashambulizi.

Lakini watu wengi hapa nchini hufundisha kinyume na taratibu hizi za kitaalam.
Mbaya zaidi wanafunzi hufundishwa kushambulia pasipo na tahadhari.
Mashambulizi ya karate ni lazima yadhibitiwe na yule anayeshambulia
ili kuondoa hatari kama kifo, kuvunjika n.k. Kuna baadhi ya wakufunzi wa karate ambao wana uwezo
mkubwa wa kutoa uhai wa mtu kwa pigo moja tu. Watu wa namna hii wanaelewa hatari iliyopo katika
kumite na siku zote hudhibiti mashambulizi yao kuepusha hizo hatari ikiwa ni pamoja na kuifanya
karate kama sanaa ambayo mtu yeyote ataweza kujifunza pasipo kujali jinsia, umri, umbo au nguvu
aliyonayo.

Tukirudi kwenye falsafa ya karate kumite niliyo izungumzia hapo juu ni 20% ya kumite halisi
katika karate. Asilimia themanini iliyobaki ni mapigano baina na wewe na madhaifu yako . Hii ndiyo
kumite ya kweli inayo kamilisha maana ya karate-do. Kila mtu ni mdhaifu wa jambo fulani, laweza
kuwa moja au zaidi. Hivyo basi ni vema tukaishi tukiyapunguza madhaifu yetu katika safari ya maisha
yetu.



MSIBA WA KARATEKA SAMSON MWAMANDA

Tunasikitika kutangaza kifo cha karateka mwenzetu, Samson Mwamanda (green belt) aliyefariki
dunia ghafla usiku wa kuamkia tarehe 27/01/2010 baada ya kuugua kwa muda mfupi.
Ijapokuwa sisi tulimpenda sana lakini Mungu alimpenda zaidi.
Tunatoa pole kwa familia, ndugu jamaa na marafiki wa marehemu.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi.
Amina



Pichani mdogo wetu Samson Mwamanda wa kwanza kutoka kulia(walio kaa)

No comments:

Post a Comment