Friday, January 15, 2010

BAADHI YA SABABU ZA STAILI NYINGI ZA KARATE KUCHEZWA PEKU(PASIPO VIATU)

i)Utamaduni wa wajapani.
Wajapani huvua viatu kabla ya kuingia kwenye nyumba zao. Hivyo basi kutokana na kwamba
karate imechukua sehemu kubwa sana ya utamaduni wa wajapani, kuvua viatu kabla ya
mafunzo ni itifaki mojawapo inayopaswa kuzingatiwa. Baadhi ya itifaki nyingine ni kusalimia
au kutoa heshima kwa kuinamisha kichwa, kutamka mbinu za karate kwa lugha ya kijapani n.k.

ii)Kuimarisha miguu.
Hii ni pamoja na kuongeza usugu na unene wa ngozi ya mguu.

iii)Kupunguza eneo la sehemu ya mguu inayoshambulia.
Kwenye fizikia imedhihirishwa kwamba mgandamizo huongezeka kutokana na kupungua kwa
eneo
. Hivyo basi ili kuongeza madhara ya shambulizi katika shabaha au eneo lililokusudiwa, ni
vyema eneo la kushambulia likapunguzwa kadri iwezekanavyo.

iv)Msafirisho wa nishati(ki) kutoka ardhini.
Mgusano baina ya unyayo na ardhi hurahisisha usafirishaji wa nishati isiyoelezeka kwa urahisi kutoka
ardhini na kuingia kwenye mwili. Ukufunzi wangu hautoshi katika kulielezea jambo hili.

KIHON NI NINI?
Kihon ni neno la kijapani linalo maanisha mbinu za msingi. Hii ni pamoja na upigaji wa ngumi au teke,
namna ya kupangua ngumi au teke, matumizi ya sehemu mbalimbali za mwili katika ushambuliaji.

SENPAI au SEMPAI NI NANI ?
Senpai ni neno la kijapani lenye maana ya mtu anaye simamia mafunzo ya karate kwa niaba ya Sensei.
Sen’ maana yake ni ‘kabla’ kama ilivyo kwa Sensei na ‘pai’ maana yake ni ‘kundi’. Hivyo senpai ni mtu
anayesimamia kundi fulani kutokana na kwamba ni mjuzi wa maarifa kuliko walio wengi katika kundi.

No comments:

Post a Comment