Saturday, June 5, 2010

MJUE SENSEI MIKIO YAHARA

SENSEI YAHARA AKIWA KWENYE 'UNSU'

SENSEI MIKIO YAHARA KATIKA 'MAKIWARA'

Mikio Yahara ni moja ya walimu hodari na waliojizolea umaarufu katika ulimwengu wa Karate.

Makarateka wengi waliokutana nae katika programu za Karate, huelezea ni kwa kiasi gani anaweza

kutumia mbinu ambazo ni ngumu kufikirika lakini pia ni kwa namna gani anaweza kuwa 'mkatili' na

mwenye 'kuogopesha' katika makabiliano.



Mikio Yahara alizaliwa mwaka 1947, huko Ehime, Japani. Alimaliza masomo yake ya elimu ya juu

katika chuo kikuu cha Kokushinkan, ambako pia alijiunga na kozi maarufu ya ualimu ya JKA.


Mikio pia anaheshimika kwa uwezo aliouonyesha katika 'Unsu', jinsi anavyo tumia nishati, wepesi

na morali kuanzia mwanzo mpaka mwisho wa kata.


Mwaka 2000, Yahara alianzisha shirikisho lake liitwalo Karatenomichi World Federation baada

ya kutoka kwenye migogoro ya JKA.

Falsafa ya shirikisho lake ni 'shambulizi la kuua' au 'hikken hisatsu'.

Imelenga katika kuimarisha mashambulizi ya karateka na hatimaye kufikia uwezo wa kuua kwa shambulizi

moja tu.


Pamoja na tofauti zetu, lakini hatuwezi kukataa uhodari aliouonyesha Sensei Mikio Yahara katika

sanaa hii ya mapigano.

No comments:

Post a Comment