Saturday, June 5, 2010

HIP!.....HIP!....HIP!!!

Kimsingi, mbinu yoyote ya Karate inatakiwa ihusishe 'hip' au kiuno kwa Kiswahili chepesi.

Walimu wa kale wa Karate walizoea kusema "kinga kwa kutumia 'hip', piga ngumi kwa kutumia 'hip',

piga teke kwa kutumia 'hip'.....".


'Hip' inatoa mchango mkubwa sana wa nishati katika shambulizi kama ikitumiwa vizuri.

Alkadhalika, matumizi ya 'hip' husaidia shambulizi kufika kwenye shabaha iliyo kusudiwa.

Kunawakati karateka hushambulia lakini kwasababu hakutumia 'hip', shambulizi lake huweza

kuishia hewani na hivyo kupoteza nishati pasipo sababu.

Lakini kamwe ustadi wake si wa kuumudu kwa siku mbili au miezi. Ni ustadi ambao karateka

anapaswa kuutafuta kwa miaka ili ifike wakati ambapo ataweza kuuonyesha hata pasipo tahadhari.

Inakuwa ni kawaida yake kutumia 'hip' katika kila mbinu ya Karate anayoitumia.

Hiyo pia huonyesha ni kwa-kiasi gani karateka huyo alivyo 'balehe' kwenye sanaa ya mapigano.

HATUA YA KWANZA YA MZUNGUKO WA 'HIP'

HATUA YA PILI YA MZUNGUKO WA 'HIP'


MWISHO WA SHAMBULIZI

No comments:

Post a Comment