Saturday, April 10, 2010

"K 3" ZA KARATE

Kumite ni moja ya tawi la karate ambalo huwavutia sana watu wanaoanza mafunzo ya karate, na hata
watu wanaopenda sanaa za mapigano kwa ujumla wake. Zaidi ya asilimia sabini ya wanafunzi wanaoanza
mafunzo ya karate hutaka kufundishwa namna ya kupigana haraka iwezekanavyo. Na hii ni moja ya
sababu kuu zinazo sababisha mbinu za msingi (kihon) kufanywa kwa uchache sana na pasipo uangalifu.

Hata mimi binafsi nilifurahi nilipokua napewa fursa ya kushiriki kwenye kumite, na nikawaida kwa
mwanafunzi yeyote aliye kwenye mikanda ya awali. Hivyo ni jukumu la mwalimu kuhakikisha kwamba
"K" tatu za karate (kihon, kata na kumite) zinafanywa kiusahihi na kwa uwiano sahihi ili kuepusha
wanafunzi kuelemea upande mmoja na kusahau "K" nyingine, kwani hizo "K" tatu ni kama magurudumu ya
bajaji nikiwa namaanisha hakuna inayopaswa kuachwa.

Kuna wanafunzi wanaodhani kwamba baada ya kujua namna ya kujihami au kumite basi tayari wanakuwa
wameishajua kila kitu kuhusiana na karate. Na kuna baadhi yao hupunguza hata mahudhurio katika dojo.
Haya ni makosa makubwa sana kwenye karate.

Ijapokuwa tunasisitiza mwanafunzi kufundishwa "K" tatu kwa usahihi lakini kiufundi "kata" na "kihon"
ni zakutiliwa mkazo zaidi katika mafunzo. Hiyo haimaanishi tuisahau kumite, la hasha. Mara nyingi
walimu wataalamu na wenye uzoefu huweza kuangalia "kata" ya mwanafunzi na kuweza kuainisha ikiwa
ni pamoja na kujua "kihon" au "kumite" yake itakuwaje. Lakini inaweza kuwawia vigumu kupata uelewa
wa "kata" na "kihon" ya mwanafunzi kwa kuangalia "kumite" yake. Na walimu wakubwa wengi hupenda
kujaji uwezo wa karateka kwa kuangalia "kata". Kata ni kipimo rahisi kuliko vyote katika kutambua
kiwango cha karateka. Kata mbovu, moja kwa moja huashiria kiwango kibovu na ufinyu wa taaluma.
Hakuna uvungu wa kujificha katika "kata".

Hii mada ni ndefu sana na inaweza kutoa maswali mengi haswa kwa wapenda "kupigana" lakini kwa leo
wacha niishie hapa.

No comments:

Post a Comment