Friday, April 16, 2010

FALSAFA ZA SENSEI SHIGERU EGAMI KUHUSIANA NA MAFUNZO YA SANAA ZA MAPIGANO

Huko China, magombo mwawili marufu kuhusu sanaa za mapigano ni Ekkin Gyo na Ekkin Zenkui.
Wanazuoni wengi wanaamini kwamba Daruma(Bodhi Dharma) ndiye aliye viandika vitabu hivyo katika
hekalu la Shaolin. Magombo haya yanaeleza ni kwa namna gani mtu anatakiwa kujifunza huku akiitakasa
nafsi yake.

Inaaminiwa kwamba Karate-do ilizaliwa kutoka kwenye mtazamo huu.

Kwa mafunzo na mazoezi, matatizo hupata suluhu.

Adui wa kwanza ni nafsi yako!

Lengo kuu la Karate-Do ni kupigania mwenendo sahihi wa tabia(kupigania tabia njema).

Ukijaribu kuyapunguza madhaifu yako katika kila siku ya maisha yako.

Ni nini maana ya upatanisho? Ni nini maana ya maisha? Amani ni nini? Umoja ni nini?

Natamani kuelewa uhusiano baina ya watu, baina ya watu na uasili wa mazingira yao.

Mwili na roho ni kitu kimoja.

Uimarishwaji wa mwili hukuza akili. Mwili uliozorota huzorotesha akili. Hiyo ndiyo sababu kuu iliyo
msukuma Daruma(Bodhi Dharma) kuanzisha mafunzo ya sanaa za mapigano katika hekalu la Shaolin takriban
miaka 1500 iliyopita.

Ni kwa mazoezi ndipo utapomudu ustadi wa mbinu. Lakini kamwe lengo la jitihada zako halitakiwi liwe
ni kujionyesha au Kupoteza amani.

Kutokana na uasili wa binadamu, ni vigumu mno akaishi peke yake. Binadamu anahitaji utulivu wa nafsi
lakini wakati huohuo anawajibika kuwapa amani wale wanaomzunguka. Atatakiwa awatendee wengine kama
ambavyo yeye angependa kutendewa. Unajaribu kuwaelewa wengine kwa kuielewa nafsi yako kwanza.

Hii ndio njia ya mafunzo. Natumaini wote tutajifunza huku tukizikagua nafsi zetu katika kupigania
mwenendo sahihi wa tabia.

No comments:

Post a Comment