MIONGOZO 22 YA MEIJIN GICHIN FUNAKOSHI
1. Karate huanza na kumalizika kwa nidhamu.
2. Daima fikiri kiubunifu.
3. Fikra huja kabla ya mwili.
4. Jiweke tayari kuwa huru kifikra.
5. Jitambue kwanza ndio uwatambue wengine.
6. Karate ni muongozo wa haki na inapaswa kutumika hivyo tu.
7. Sogea kufuatana na mpinzani wako.
8. Kamae ni kwa wanafunzi wapya na shizentai ni kwa wazoefu.
9. Usifikirie kwamba inabidi ushinde ila fikiri kwamba hupaswi kushindwa.
10. Karate si katika Dojo peke yake.
11. Husisha karate katika kila jambo ulifanyalo, wakati wote fikiri kuitumia miongozo hii kila siku.
12. Mafunzo ya karate ni ya wakati wote wa maisha yako.
13. Karate ni kama maji ya moto, yasipoendelea kupashwa moto au kuhifadhiwa na joto lake, hupoa.
14. Mara tu utokapo nyumbani, una wapinzani zaidi ya elfu moja.
15. Hakuna shambulio la kwanza kwenye karate.
16. Elewa tofauti ya sehemu zenye madhara na zisizo na madhara.
17. Uzembe huja kabla ya ajali.
18. Fikiri mikono na miguu yako kuwa kama sime.
19. Kumbuka vipengele vigumu na vyepesi kwenye kata.
20. Karate ikifanyika vyema ni tofauti na kombati(struggle fighting).
21. Jihadhari na matendo yako, usije ingia matatani.
22. Mafunzo ya kata si uhalisi wa jambo lenyewe.
Friday, February 19, 2010
Friday, February 5, 2010
NINI MAANA YA KUMITE ?
Sehemu nyingine ya mafunzo ya karate hujumuisha makabiliano baina ya wanafunzi, hii kwa neno
la kijapani huitwa kumite. Kumite hufundishwa kwa hatua mbalimbali kutegemea na staili ya karate.
Kimsingi wanafunzi hujifunza ustadi sahihi wa kushambulia na kuyakabili mashambulizi katika mikanda
ya awali kabla ya kuruhusiwa kukabiliana wakiwa huru kushambulia na kujikinga na mashambulizi.
Lakini watu wengi hapa nchini hufundisha kinyume na taratibu hizi za kitaalam.
Mbaya zaidi wanafunzi hufundishwa kushambulia pasipo na tahadhari.
Mashambulizi ya karate ni lazima yadhibitiwe na yule anayeshambulia
ili kuondoa hatari kama kifo, kuvunjika n.k. Kuna baadhi ya wakufunzi wa karate ambao wana uwezo
mkubwa wa kutoa uhai wa mtu kwa pigo moja tu. Watu wa namna hii wanaelewa hatari iliyopo katika
kumite na siku zote hudhibiti mashambulizi yao kuepusha hizo hatari ikiwa ni pamoja na kuifanya
karate kama sanaa ambayo mtu yeyote ataweza kujifunza pasipo kujali jinsia, umri, umbo au nguvu
aliyonayo.
Tukirudi kwenye falsafa ya karate kumite niliyo izungumzia hapo juu ni 20% ya kumite halisi
katika karate. Asilimia themanini iliyobaki ni mapigano baina na wewe na madhaifu yako . Hii ndiyo
kumite ya kweli inayo kamilisha maana ya karate-do. Kila mtu ni mdhaifu wa jambo fulani, laweza
kuwa moja au zaidi. Hivyo basi ni vema tukaishi tukiyapunguza madhaifu yetu katika safari ya maisha
yetu.
MSIBA WA KARATEKA SAMSON MWAMANDA
Tunasikitika kutangaza kifo cha karateka mwenzetu, Samson Mwamanda (green belt) aliyefariki
dunia ghafla usiku wa kuamkia tarehe 27/01/2010 baada ya kuugua kwa muda mfupi.
Ijapokuwa sisi tulimpenda sana lakini Mungu alimpenda zaidi.
Tunatoa pole kwa familia, ndugu jamaa na marafiki wa marehemu.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi.
Amina

Pichani mdogo wetu Samson Mwamanda wa kwanza kutoka kulia(walio kaa)
la kijapani huitwa kumite. Kumite hufundishwa kwa hatua mbalimbali kutegemea na staili ya karate.
Kimsingi wanafunzi hujifunza ustadi sahihi wa kushambulia na kuyakabili mashambulizi katika mikanda
ya awali kabla ya kuruhusiwa kukabiliana wakiwa huru kushambulia na kujikinga na mashambulizi.
Lakini watu wengi hapa nchini hufundisha kinyume na taratibu hizi za kitaalam.
Mbaya zaidi wanafunzi hufundishwa kushambulia pasipo na tahadhari.
Mashambulizi ya karate ni lazima yadhibitiwe na yule anayeshambulia
ili kuondoa hatari kama kifo, kuvunjika n.k. Kuna baadhi ya wakufunzi wa karate ambao wana uwezo
mkubwa wa kutoa uhai wa mtu kwa pigo moja tu. Watu wa namna hii wanaelewa hatari iliyopo katika
kumite na siku zote hudhibiti mashambulizi yao kuepusha hizo hatari ikiwa ni pamoja na kuifanya
karate kama sanaa ambayo mtu yeyote ataweza kujifunza pasipo kujali jinsia, umri, umbo au nguvu
aliyonayo.
Tukirudi kwenye falsafa ya karate kumite niliyo izungumzia hapo juu ni 20% ya kumite halisi
katika karate. Asilimia themanini iliyobaki ni mapigano baina na wewe na madhaifu yako . Hii ndiyo
kumite ya kweli inayo kamilisha maana ya karate-do. Kila mtu ni mdhaifu wa jambo fulani, laweza
kuwa moja au zaidi. Hivyo basi ni vema tukaishi tukiyapunguza madhaifu yetu katika safari ya maisha
yetu.
MSIBA WA KARATEKA SAMSON MWAMANDA
Tunasikitika kutangaza kifo cha karateka mwenzetu, Samson Mwamanda (green belt) aliyefariki
dunia ghafla usiku wa kuamkia tarehe 27/01/2010 baada ya kuugua kwa muda mfupi.
Ijapokuwa sisi tulimpenda sana lakini Mungu alimpenda zaidi.
Tunatoa pole kwa familia, ndugu jamaa na marafiki wa marehemu.
Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi.
Amina

Pichani mdogo wetu Samson Mwamanda wa kwanza kutoka kulia(walio kaa)
Friday, January 15, 2010
BAADHI YA SABABU ZA STAILI NYINGI ZA KARATE KUCHEZWA PEKU(PASIPO VIATU)
i)Utamaduni wa wajapani.
Wajapani huvua viatu kabla ya kuingia kwenye nyumba zao. Hivyo basi kutokana na kwamba
karate imechukua sehemu kubwa sana ya utamaduni wa wajapani, kuvua viatu kabla ya
mafunzo ni itifaki mojawapo inayopaswa kuzingatiwa. Baadhi ya itifaki nyingine ni kusalimia
au kutoa heshima kwa kuinamisha kichwa, kutamka mbinu za karate kwa lugha ya kijapani n.k.
ii)Kuimarisha miguu.
Hii ni pamoja na kuongeza usugu na unene wa ngozi ya mguu.
iii)Kupunguza eneo la sehemu ya mguu inayoshambulia.
Kwenye fizikia imedhihirishwa kwamba mgandamizo huongezeka kutokana na kupungua kwa
eneo. Hivyo basi ili kuongeza madhara ya shambulizi katika shabaha au eneo lililokusudiwa, ni
vyema eneo la kushambulia likapunguzwa kadri iwezekanavyo.
iv)Msafirisho wa nishati(ki) kutoka ardhini.
Mgusano baina ya unyayo na ardhi hurahisisha usafirishaji wa nishati isiyoelezeka kwa urahisi kutoka
ardhini na kuingia kwenye mwili. Ukufunzi wangu hautoshi katika kulielezea jambo hili.
KIHON NI NINI?
Kihon ni neno la kijapani linalo maanisha mbinu za msingi. Hii ni pamoja na upigaji wa ngumi au teke,
namna ya kupangua ngumi au teke, matumizi ya sehemu mbalimbali za mwili katika ushambuliaji.
SENPAI au SEMPAI NI NANI ?
Senpai ni neno la kijapani lenye maana ya mtu anaye simamia mafunzo ya karate kwa niaba ya Sensei.
‘Sen’ maana yake ni ‘kabla’ kama ilivyo kwa Sensei na ‘pai’ maana yake ni ‘kundi’. Hivyo senpai ni mtu
anayesimamia kundi fulani kutokana na kwamba ni mjuzi wa maarifa kuliko walio wengi katika kundi.
i)Utamaduni wa wajapani.
Wajapani huvua viatu kabla ya kuingia kwenye nyumba zao. Hivyo basi kutokana na kwamba
karate imechukua sehemu kubwa sana ya utamaduni wa wajapani, kuvua viatu kabla ya
mafunzo ni itifaki mojawapo inayopaswa kuzingatiwa. Baadhi ya itifaki nyingine ni kusalimia
au kutoa heshima kwa kuinamisha kichwa, kutamka mbinu za karate kwa lugha ya kijapani n.k.
ii)Kuimarisha miguu.
Hii ni pamoja na kuongeza usugu na unene wa ngozi ya mguu.
iii)Kupunguza eneo la sehemu ya mguu inayoshambulia.
Kwenye fizikia imedhihirishwa kwamba mgandamizo huongezeka kutokana na kupungua kwa
eneo. Hivyo basi ili kuongeza madhara ya shambulizi katika shabaha au eneo lililokusudiwa, ni
vyema eneo la kushambulia likapunguzwa kadri iwezekanavyo.
iv)Msafirisho wa nishati(ki) kutoka ardhini.
Mgusano baina ya unyayo na ardhi hurahisisha usafirishaji wa nishati isiyoelezeka kwa urahisi kutoka
ardhini na kuingia kwenye mwili. Ukufunzi wangu hautoshi katika kulielezea jambo hili.
KIHON NI NINI?
Kihon ni neno la kijapani linalo maanisha mbinu za msingi. Hii ni pamoja na upigaji wa ngumi au teke,
namna ya kupangua ngumi au teke, matumizi ya sehemu mbalimbali za mwili katika ushambuliaji.
SENPAI au SEMPAI NI NANI ?
Senpai ni neno la kijapani lenye maana ya mtu anaye simamia mafunzo ya karate kwa niaba ya Sensei.
‘Sen’ maana yake ni ‘kabla’ kama ilivyo kwa Sensei na ‘pai’ maana yake ni ‘kundi’. Hivyo senpai ni mtu
anayesimamia kundi fulani kutokana na kwamba ni mjuzi wa maarifa kuliko walio wengi katika kundi.
Saturday, January 9, 2010
MUHTASARI WA MASHINDANO YA KATA ITALY
MAANA YA KATA KATIKA KARATE
Kata ni makabiliano ya kufikirika baina ya karateka na wapinzani kutoka pande mbalimbali.
Tunatumia neno wapinzani badala ya maadui kwa sababu kwenye falsafa za karate hatuna adui.
Kila staili ya karate ina kata zake ijapokuwa baadhi zinafanana kiustadi, majina n.k.
Vipengele vitatu muhimu ambavyo karateka anapaswa kuvizingatia pindi aichezapo kata:
i)Nidhamu katika matumizi ya nguvu. Nguvu kuu inapaswa kutumika katika ile sekunde
ya shambulizi tu, baada ya shambulizi karateka atatakiwa kutoka katika hali ya ukakamavu
ili kuepuka uzalishaji wa nguvu isiyo na matumizi na hatimaye kupoteza nguvu bila sababu.
Lakini kuna kata kama hangetsu au kata nyingi za gojyu-ryu ambazo humtaka karateka
kukakamaa kuanzia mwanzo wa kata mpaka mwisho. Hapo kipengele cha kwanza si lazima
kipewe kipaumbele.
ii)Udhibiti wa spidi ya mbinu. Karateka anapaswa kutambua vyema ni mbinu gani katika kata
zinapaswa kufanywa taratibu na zipi atatakiwa kuzifanya haraka iwezekanavyo, hii pia hutumika
katika kuijua spidi ya karateka. Kama ilivyo kwa mwanamichezo au msanii, karateka anatakiwa
audhibiti mwili wake na si mwili umdhibiti yeye.
iii)Mikao na hatua sahihi pamoja na upumuaji.
Mikao na hatua katika kata ni lazima viwe sahihi ili kutoa tafsiri sahihi ya kata. Lakini pia namna
ya upumuaji ni kitu muhimu mno hasa katika viwango vya juu sana kwenye karate. Kuna wakati
upumuaji hupewa kipaumbele kuliko mbinu ya karate kwa sababu pumzi ni uhai. Upumuaji
mzuri utamsaidia sana karateka katika matumizi ya nguvu na kumfanya aweze kudumu kwenye
zoezi au pambano kwa muda mrefu.
Hivyo ni vipengele muhimu sana katika kata, vipengele vingine muhimu ni kama ; uzatiti wa wazo katika mbinu, mtikiso wa kiuno, kutanuka na kusinyaa kwa mwili na hatua, uelekeo, mlio wa shambulizi(kiai ), nidhamu, shabaha ya mbinu, stemina, muda, kujiamini, morali, tahadhari (zashin) na kadhalika.
Friday, January 8, 2010
SENSEI NI NANI ?
Huko Japani kila mwalimu huitwa Sensei. Lakini pia mwanasheria au daktari huitwa Sensei kutokana na
kwamba ni msomi au mjuzi wa maarifa kuliko walio wengi.Pia kama ilivyo ada kwamba wanasheria wengi hujihusisha na maswala ya siasa hivyo huko Japani kunawakati mwanasiasa pia huitwa Sensei .
Lakini labda wengi wamewahi kujiuliza kwamba ni sifa zipi hasa zinazomfanya mtu awe Sensei?
Watu wanaoitwa Sensei wanatakiwa kuishi kama walimu katika maisha yao yote.
Kimsingi neno Sensei limetokana na maneno mawili ya kijapani yaani ‘sen’ na ‘sei’.
i) ’sen’ maana yake ni kabla.
ii)’sei’ maana yake ni kuzaliwa.
Hivyo Sensei ni mtu ambaye amezaliwa kabla(kifikra) au mtu aliyepata ujuzi wa jambo fulani kabla ya
wengine. Heshima ni moja ya vigezo vikubwa sana kwa mtu anayeitwa Sensei.
Anatakiwa kuheshimu kila kiumbe chenye uhai. Hii ni kwa sababu heshima ni kitu muhimu sana
katika kujenga uhusiano mzuri miongoni mwa viumbe hai akiwemo binadamu.
Mara nyingi kwenye karate cheo cha usensei hutolewa katika mazingira yafuatayo :-
1)Karateka aliye kwenye daraja la mkanda mweusi na ana wanafunzi ambao yeye kama mwalimu
huwafundisha na kuyaishi yale anayoyafundisha. Huyu anapaswa kuitwa Sensei haswa na wanafunzi
wake. Si lazima kuitwa Sensei na kila karateka ila wanafunzi wake.
2)Karateka aliye kwenye daraja la mkanda mweusi na aliyeteuliwa na shirikisho fulani la kitaifa
au kimataifa kuwa Sensei. Huyu kwa heshima na taadhima anapaswa kutambuliwa kama
Sensei na karateka yeyote.
Huko Japani kila mwalimu huitwa Sensei. Lakini pia mwanasheria au daktari huitwa Sensei kutokana na
kwamba ni msomi au mjuzi wa maarifa kuliko walio wengi.Pia kama ilivyo ada kwamba wanasheria wengi hujihusisha na maswala ya siasa hivyo huko Japani kunawakati mwanasiasa pia huitwa Sensei .
Lakini labda wengi wamewahi kujiuliza kwamba ni sifa zipi hasa zinazomfanya mtu awe Sensei?
Watu wanaoitwa Sensei wanatakiwa kuishi kama walimu katika maisha yao yote.
Kimsingi neno Sensei limetokana na maneno mawili ya kijapani yaani ‘sen’ na ‘sei’.
i) ’sen’ maana yake ni kabla.
ii)’sei’ maana yake ni kuzaliwa.
Hivyo Sensei ni mtu ambaye amezaliwa kabla(kifikra) au mtu aliyepata ujuzi wa jambo fulani kabla ya
wengine. Heshima ni moja ya vigezo vikubwa sana kwa mtu anayeitwa Sensei.
Anatakiwa kuheshimu kila kiumbe chenye uhai. Hii ni kwa sababu heshima ni kitu muhimu sana
katika kujenga uhusiano mzuri miongoni mwa viumbe hai akiwemo binadamu.
Mara nyingi kwenye karate cheo cha usensei hutolewa katika mazingira yafuatayo :-
1)Karateka aliye kwenye daraja la mkanda mweusi na ana wanafunzi ambao yeye kama mwalimu
huwafundisha na kuyaishi yale anayoyafundisha. Huyu anapaswa kuitwa Sensei haswa na wanafunzi
wake. Si lazima kuitwa Sensei na kila karateka ila wanafunzi wake.
2)Karateka aliye kwenye daraja la mkanda mweusi na aliyeteuliwa na shirikisho fulani la kitaifa
au kimataifa kuwa Sensei. Huyu kwa heshima na taadhima anapaswa kutambuliwa kama
Sensei na karateka yeyote.
Tuesday, January 5, 2010
Subscribe to:
Posts (Atom)