Thursday, January 20, 2011

JIYU IPPON KUMITE NA SENSEI LEFEVRE

VITENDEA KAZI VYA SHINDANO

1. Vibendera vyeupe na vyekundu (5 kwenye pambano).

2. Mbao za alama (7 kwenye pambano).

3. Vifaa vya rekodi (madaftari n.k).

4. Vifaa vya muda.

5. Mikanda myeupe/yabluu na myekundu.

6. Glovu.

7. Filimbi (5 kwenye pambano).

STAFU YA SHINDANO

1. Mratibu wa Shindano:
Atakuwa na jukumu la kusimamia mwenendo mzima wa shindano na
kuhakikisha kila kitu kinaenda kama ilivyopangwa. Majukumu yake
hayato takiwa kuingilia sheria na taratibu za uchezeshaji wa shindano.

2. Daktari wa shindano:
Atasimamia maswala yote yanayohusika na matibabu katika shindano.

3. Timu ya Huduma ya Kwanza (First Aid):
Watatakiwa kuwa tayari kwa tatizo lolote la kiafya linaloweza kujitokeza
katika shindano kwa kusaidiana na Daktari wa shindano.